Image
Image

Nyalandu aomba Waziri wa maliasili Prof.Maghembe asaidiwe.

“Watendaji ni kiungo muhimu kwa waziri kutekeleza majukumu yake, ni matumaini yangu mtampa ushirikiano katika hili,” alisema.
Nyalandu alisema ushirikiano huo utawezesha rasilimali za nchi kama misitu na wanyama kuendelea kuwapo na kutumika kwa njia endelevu.
Alisema umuhimu wa wizara kuendelea kutangaza vivutio vya utalii ili kuhakikisha malengo katika sekta hiyo unazidi kufikiwa.
“Wizara hii ina watendaji wema na wanaojitolea kutimiza majukumu yao, kuna askari wa wanyamapori na misitu wanaofanya kazi kwa weledi,” alisema Nyalandu.
Kwa upande wake, Waziri Maghembe alisema wizara yake imejipanga kufanya kazi kwa kasi zaidi na kuendeleza yale ambayo yalifanywa na mtangulizi wake.
“Ninatambua mwenzangu alifanya kazi kubwa ya  kuendeleza na kusimamia wizara… na mimi kwa kushirikiana na watendaji tutafanya kazi na kuzidi kuleta mafanikio,” alisema Profesa Maghembe.
Alitaja baadhi ya maeneo yatakayopewa kipaumbele ni kukomesha wizi wa magogo na vita dhidi ya ujangili wa wanyama pori.
“Watu walikuwa wanavuna magogo na kujifanya kama yanatoka nchi jirani ya Zambia, ulipambana na kutengeneza ushirikiano na nchi hizo…tutaiga mfano wako,” alisema.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment