Image
Image

Waziri wa zamani Rwanda kukaa jela miaka 47.

Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR) imeamua waziri mmoja wa zamani wa Rwanda atumikie kifungo cha miaka 47 jela kwa mchango wake mauaji ya kimbari ya 1994.
Pauline Nyiramasuhuko ni mmoja wa washtakiwa sita waliokuwa wamekata rufaa kwenye mahakama hiyo maalum ambayo imemaliza kazi yake.
Alikuwa amehukumiwa kifungo cha maisha gerezani awali, lakini mahakama ikaamua kupunguza adhabu dhidi yake, sawa na adhabu dhidi ya Arsène Shaim Ntahobali na Elie Ndayambaje.
Kesi hizo zilikuwa za mwisho kusikizwa na mahakama hiyo kabla ya kufungwa rasmi baada ya kusikiza kesi dhidi ya washukiwa wa mauaji hayo kutoka mjini Arusha, Tanzania kwa miaka 21.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment