Image
Image

Wenger:Tuna fursa dhidi ya Barcelona.

Wachezaji wa safu ya kiungo cha kati wa Arsenal Mesut Ozil na Aaron Ramsey pamoja na kipa Petr Cech watarudi katika mechi ya vilabu bingwa Ulaya dhidi ya mabingwa watetezi Barcelona siku ya jumanne.
Wachezaji hao walipumzishwa katika mechi ya kombe la FA siku ya Jumamosi dhidi ya Hull City.
Barca itamrudisha katika kikosi chake beki Gerard Pique,ambaye alipumzishwa katika ushindi dhidi ya Las Palmas na kiungo wa kati Sergio Busquets ambaye alikuwa akihudumia marufuku.
''Tunahitaji kuwa na mwelekeo katika mechi hiyo kwa pamoja ili kuwa na fursa ,''alisema mkufunzi wa Arsenal Arsene Wenger.
Arsenal iliondolewa na kilabu ya Monaco katika mchujo wa msimu uliopita.
Walipoteza kwa mabao 3-1 katika uwanja wa Emirates,lakini wakashindwa kufuzu baada ya kushinda maba 2-0 ugenini kutokana na bao la ugenini.
''Ni fursa kuonyesha kwamba tumepata funzo,kwa sababu tulijipatia kibarua kigumu baada ya mechi ya nyumbani,''alisema.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment