Image
Image

Mwijage kuwabana wafanya biashara wanao wanyonya wakulima.

Akijibu Maswali ya Wabunge Mjini Dodoma, katika kipindi cha maswali na majibu,Waziri wa Wizara hiyo Mhe.Charles Mwijage amesema kila wilaya ianzishe mitaa ya viwanda ili kuwasaidia wakulima kunufaika na mazao yao kwa kudhibiti udanganyifu unaofanywa na wafanyabiashara kwa kuwanyonya wakulima.
Mhe. Mwijage amesema kuwa atalazimika kununua mizani pamoja na mashine za EFDS na kuweka vituo vya mauzo hayo ili kuleta tija kwa wakulima huku akiongeza kwa kusema kuwa sasa kutakuwa na kipimo maalumu cha uzito wa kufunga mizigo yao.
Kwa upande mwingine,akizungumzia viwanda vilivyobinafsishwa, Mhe.Mwijage amesema wawekezaji wote waliopewa viwanda na wameshindwa kuviendeleza serikali inawataka wavirudishe mara moja.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment