Image
Image

Zoezi la kuondoka kwa waasi na raia kutoka Mashariki mwa Mji wa Aleppo giza totoro.

Zoezi la kuondoka kwa waasi na raia kutoka Mashariki mwa Mji wa Aleppo limecheleweshwa kwa sababu ambazo hazijawekwa wazi.
Mabasi yaliyokuwa yamejaa watu yalikuwa yaanze kuondoka alfajiri ya leo ikiwa ni sehemu ya makubaliano  na Serikali ya Syria ambayo vikosi vyake vinaudhibiti Mji wa Aleppo bada ya mapigano makali.
Kwa mujibu wa Shirika la Kutetea Haki za Binadamu la Syria lenye makao yake  nchini Uingereza, hakuna muasi au raia aliyeondoka Mashariki mwa Aleppo saa kumi-na-moja alfajiri kama ilivyotakiwa.
Wanamgambo  1,500  wamesalimisha silaha zao kwenye  vitongoji vya Kusini mwa Mji Mkuu wa Syria  Damascus   chini ya sheria ya msamaha  uliotolewa na Serikali ya Rais  BASHAR al-ASSAD  mapema mwaka huu .
Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kiarabu la  Syriam,-SANA- wapiganaji hao waliokuwa na silaha wamesalimisha silaha zao katika Kijiji cha  Kanaker , kwenye Jimbo la  Rif Dimashq  na kupelekwa kwenye kituo cha kupewa nasaha.
Chini ya sheria hiyo watakaosalimisha silaha zao ambazo walikuwa wakimiliki kwa sababu moja au nyingine wanaweza kusamehewa.


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment