Image
Image

Zitto Kabwe ang'aka mauaji mengine Kibiti, Afisa mtendaji na Mwenyekiti wake wapigwa risasi.

Watu 2 wanahofiwa kuuawa kwa kupigwa risasi katika kijiji cha Mangwi wilayani Kibiti kuamkia leo, Kamanda Lyanga amesema wanafuatilia tukio hilo ili kujua ukweli wake.
Kufuatia taarifa hizo za kuuawa kwa watu wawili Mbunge wa Kigoma mjini Mhe. Zitto Kabwe amefunguka juu ya mauaji yanayoendelea kutokea mkoa wa Pwani eneo la Kibiti kwa kuitaka serikali itazame jambo hilo kwa mtazamo mpana kwa kuwa wananchi wana haki ya kujua nini kinachoendelea juu ya mauaji hayo.
Zitto amebainisha hayo kupitia ukurasa wake Facebook huku akidai kuwa Usiku wa kuamkia leo yameweza kutokea mauaji mengine ambayo yamepelekea kuuwawa Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Mangwi kata ya Mchukwi na Mwenyekiti wake kwa kupigwa risasi na baadaye kuchomwa moto nyumba zao.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment