Image
Image

Kiongozi wa ACT Zitto Kabwe aachiwa na kukamatwa tena.

Zitto Kabwe , kiongozi mkuu wa chama cha upinzani nchini Tanzania cha ACT Wazalendo, aachiwa na kukamatwa tena kwa maelekezo ya ofisi ya afisa upelelezi imakosa ya jinai.
Mbunge huyo wa Kigoma mjini, alikamatwa mara ya kwanza asubuhi ya Jumanne nyumbani kwake mjini Dar es salaam na kupelekwa kituo cha polisi Chang'ombe.
Baada ya masaa kadhaa mbunge huyo aliachiliwa huru kabla ya kukamatwa tena.
Akizungumza na BBC, wakili wa Bwana Kabwe, Stephan Ally Mwakibolwa anasema sababu zilizotajwa kwa kushikwa kwake ni kutoa maneno yanayodaiwa kuwa ni ya uchochezi.
"Kauli kubwa haswa wanayosema ni kuihusisha serikali ya CCM na matukio ya watu waliookotwa katika fukwe za bahari ya hindi wakiwa wamefariki ,pamoja na tukio la mbunge Tundu Lissu"
Bwana Kabwe sasa amepelekwa katika kituo cha polisi cha Kamata mjini Dar es salaam.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment