WAFANYAKAZI wa Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (Tazara)
wameulalamikia uongozi wa mamlaka hiyo upande wa Tanzania kwa kujilipa
malimbikizo ya marupurupu ya miezi minne, huku ukijua kuwa watumishi
wengine hawajalipwa malimbikizo ya mshahara wa Januari mwaka huu.
Wakitoa malalamiko yao, Dar es Salaam kwa nyakati tofauti, baadhi ya
wafanyakazi hao walisema tatizo la mishahara bado ni tete kwa mamlaka
hiyo, kwani kuanzia Januari hadi sasa watumishi wengi hawajalipwa
stahiki zao ipasavyo.
“Ni kweli tulikuwa hatujalipwa mshahara kuanzia Januari mwaka huu
hadi sasa, ila tulipoona mambo yanazidi kuwa magumu, tulizungumza na
chama cha wafanyakazi (Trawu), ambao walifuatilia na serikali iliingilia
kati baadhi yetu wakalipwa Juni mwaka huu,” alisema mmoja wa
wafanyakazi hao.
Akizungumzia hilo, Kaimu Mwenyekiti wa Trawu wa Kanda, Yasin Mleki
alisema ni kweli kuna matatizo ya malimbikizo ya malipo ya mshahara,
ambao kuanzia Januari mwaka huu hadi sasa, asilimia kubwa ya watumishi
wanadai stahiki zao.
Mleki alisema kutokana na tatizo hilo, chama hicho kilizungumza na
uongozi wa Tazara ambao waliwalipa asilimia 20 ya watumishi wote
mshahara wa Januari. Wengi wa watumishi waliolipwa ni wa makao makuu,
karakana na idara ya ufundi.
“Ni kweli kuna tatizo la mishahara kutolipwa kwa wakati, mfano Juni
mwaka huu, Tazara waliwalipa baadhi ya watumishi mshahara wa Januari,
ilihali leo ni mwezi Agosti, sasa unategemea watumishi wanaishije,”
alisema Mleki.
Alisema baada ya malipo hayo ambayo hayakuweza kulipwa kwa watumishi
wote, wafanyakazi walilalamika ndipo uongozi ukafanikiwa kupata fedha
serikalini Sh bilioni 2.5 ambazo zililipa malimbikizo ya mshahara
kuanzia Februari hadi Mei mwaka huu kwa wafanyakazi wote.
Alisema katika malipo hayo serikali ililipa mshahara pekee bila
marupurupu mengine na kwamba ilipofika Agosti 12, mwaka huu uongozi wa
Tazara ulipata fedha zitokanazo na uendeshaji wa mamlaka hiyo.
Inadaiwa kwamba uongozi walijilipa fedha hizo za malimbikizo ya
marupurupu ya kuanzia Februari mwaka huu hadi Mei wakati watumishi
wengine wengi hawajalipwa mshahara wa Januari.
“Ni jambo la ajabu, watumishi karibu asilimia 80 tunadai mshahara wa
Januari ambao wenzetu wakiwemo viongozi walishajilipa, sasa kwa nini
hizo fedha zilizopatikana za ndani wasingetulipa kwanza sisi tunaodai
mshahara wa nyuma halafu marupurupu ambayo tunadai wote yaendelee kuwa
deni la wote?” alihoji Mleki.
Akizungumzia suala hilo, Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Tazara, Dk
Betram Kiswaga alisema ni kweli kuna matatizo ya ndani ya mamlaka hiyo
ambayo uongozi umekaa pamoja na Trawu na kujadili jinsi ya
kuyashughulikia
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments:
Post a Comment