Image
Image

Update:Mmoja auawa,wanne wajeruhiwa mapigano ya wakulima na wafugaji Mvomero.



MTU mmoja ameuawa na wengine wanne wakiwemo askari Polisi wawili kujeruhiwa baada ya kutokea mapigano ya wakulima na wafugaji katika kijiji cha Dihinda wilayani Mvomero mkoani Morogoro.

Taarifa zilizopatikana kutoka eneo la tukio na kuthibitishwa na Mwenyekiti wa Kijiji cha Dihinda kuwa mapigano hayo yaliibuka baada ya mfugaji mmoja wa jamii ya kimasai kudaiwa kuingiza Mifugo kwenye shamba la mazao jamii ya mikunde,la Bwana Bakari Mlunguza ambapo wakulima waliingilia kati na kuwakamata ng'ombe takribani 100 wa mfugaji huyo na kuzipeleka kwenye ofisi ya kijiji.

Ilielezwa zaidi kuwa wakiwa ofisini hapo katika kikao cha pamoja na mmiliki wa mifugo hiyo,viongozi wa kijiji na mkulima ambaye Mazao yake yanadaiwa kuliwa na Mifugo,iliamuriwa mfugaji huyo alipe  shilingi laki mbili kama fidia kwa mazao yaliyoliwa,jambo ambalo aliafiki katika kikao lakini badala yake akataka kuondoka bila kulipa fidia.

Hata hivyo wakulima walipinga kitendo hicho na kuzuia Mifugo hiyo isiondolewe kabla ya fidia,lakini kundi la wafugaji liliingilia kati na kusababisha vurugu ambapo mkulima mmoja aliuawa na wengine wawili kujeruhiwa kwa kukatwa katwa mapanga ambapo wananchi nao walivamia Mifugo iliyokuwa ikishikiliwa na kuwaua ng'ombe 72.

Wakati tukio hilo likitokea,askari polisi walifika eneo la tukio kudhibiti vurugu zilizo lakini wafugaji waliwajeruhi askari wawili na kufanya jumla ya watu wanne kujeruhiwa katika tukio hilo na kulazwa hospitali ya misheni ya Bwagala iliyopo wilayani Mvomero.

Tayari Waziri wa Kilimo,Uvuvi na Ufugaji Mwigulu Nchemba,kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Morogoro na wilaya ya Mvomero wamekwenda eneo la tukio kufahamu zaidi chanzo cha tukio hilo na kuzungumzia na wananchi wa makundi ya wakulima na wafugaji.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment